Breaking News

NIPO TAYARI KUCHUKIWA NA WANAUME WA DAR- MAKONDA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema yupo tayari kuchukiwa na wanaume wa Mkoa huo wanaokwazika na uamuzi wake wa kuwatetea wanawake, Limeripoti gazeti la mwananchi nchini Tanzania

Bwana Makonda amesema yupo tayari kuchukiwa na wanaume wa Mkoa huo wanaokwazika na uamuzi wake wa kuwatetea wanawake.



Amesema hawezi kukaa kimya kuangalia mateso ya wanawake yanayoweza kupatiwa ufumbuzi ikiwa wanaume watabadilika.

Makonda alikuwa akizungumza Jumapili katika Kanisa la Inuka Uangaze la Mtume Boniface Mwamposa maarufu 'Bulldozer' lililopo Kawe, Dar es Salaam.

Amesema wakati wa wanawake kutembea kifua mbele umefika na siku zote atasimama kuwatetea.

Usikubali kupitwa na chochote kile tembelea App hii kila mara kupata Habari zote zinazojiri Tanzania na nje ya Tanzania katika Michezo, Magazeti, Mahusiano, Elimu, Ajira, Video, Audios, Tamthilia na Udaku.