Breaking News

AZAM SASA KAMILI KUIVAA TRIANGLE FC

Baada ya kufanya maboresho katika App yetu sasa tunakuomba ufanye ku update ili kuendelea kupata habari zetu zote pamoja na kutazama mechi live, kusikiliza radio zote za Tanzania na mengine mengi katika ubora zaidi

ILI KU UPDATE BOFYA👉👉👉 HAPA 
HAKIKISHA UMEUPDATE


Awamu ya pili ya wachezaji watano wa Azam FC waliokuwa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, imewasili nchini Zimbabwe kwa ajili ya maandalizi ya kukabiliana na Triangle United.

Hivyo basi kikosi cha Azam FC kipo kamili  baada ya msafara ya kwanza kuongozwa na mkufunzi msaidizi wa timu hiyo Idd Cheche kutangulia kwaajili ya  kuweka mambo sawa.

Wachezaji hao wameungana na wenzao ambao walitangulia awali kwa ajili ya kuanza maandalizi ya mchezo wa kombe la Shirikisho utakaopigwa Septemba 28.

Wachezaji hao walibaki nchini ni wale waliotumikia timu ya taifa iliyocheza na Sudan uwanja wa Taifa mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Chan.

Wachezaji hao ni Frank Domayo ‘Chumvi’, Mudathir Yahya na Shaaban Chilunda, ambao wameanza mazoezi huku kocha Mkuu, Etienne Ndayiragije, akiwapumzisha kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na winga Idd Seleman ‘Nado’.
Zaidi Na Zaidi Tembelea App Hii Kila Mara , Kila Saa Kupata Habari Zote Zinazojiri Tanzania Na Nje Ya Tanzania Katika Mapenzi Na Mahusiano, Elimu, Ajira, Michezo, Maisha, Magazeti, Videos, Audios, Tamthilia Na Burudani.