Jeshi la Polisi Yamshikilia Halima Mdee....Kufikishwa Mahakamani Jumatatu
Mbunge wa Kawe Halima Mdee anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Oysterbay, kufuatia agizo la Mahakama ya Kisutu la kukamatwa kwa wabunge wanne wa CHADEMA.
'Ni kweli yupo hapa kituoni tunamshikilia kama ambavyo Mahakama iliagiza na yeye amekuja mwenyewe kuripoti hapa, hivyo taratibu zote za kipolisi zinafanyika na Jumatatu atafikishwa mahakami', amesema Msaidizi wa RPC Kinondoni.
Amri hiyo ya kukamatwa kwa wabunge hao Halima Mdee, Peter Msigwa, John Heche na Ester Bulaya, ilitolewa jana, Novemba 15, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo Thomas Simba, ambapo alisema kuwa kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya upande wa mashtaka kumhoji Mbowe na baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake kutoka upande wa utetezi na ndipo ilipobainika washtakiwa hao wanne kutokuwepo mahakamani.
UPDATE NIJUZE HABARI APP, CLICK HERE